Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) –ABNA– Iraq imetangaza kuwa zaidi ya mahujaji milioni 1.813 kutoka mataifa 172 tofauti wameingia nchini humo tangu kuanza kwa Mwezi Mtukufu wa Muharram kwa lengo la kushiriki Ziara ya Arbaeen ya Imam Husayn (a.s).
Mkuu wa Kitengo cha Habari za Usalama nchini Iraq, Luteni Jenerali Saad Maan, amesema kuwa hadi sasa jumla ya mahujaji 1,813,000 wamewasili nchini Iraq, huku idadi hiyo ikiendelea kuongezeka kadiri siku za kuelekea Arbaeen zinavyosogea.
Ameeleza kuwa serikali ya Iraq, kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na taasisi mbalimbali za huduma, imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha mahujaji wanapata ulinzi, usafiri, huduma za afya na mazingira salama katika safari yao ya kuelekea miji mitakatifu ya Najaf na Karbala.
Ziara ya Arbaeen ya Imam Husayn (a.s) ni miongoni mwa mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani, ikiwakusanya mamilioni ya waumini kutoka pembe mbalimbali za dunia kila mwaka kwa ajili ya kuadhimisha siku ya arobaini tangu kuuawa shahidi kwa Imam Husayn (a.s) katika tukio la Karbala.
Maoni yako